Posts

PICHA 5 ZA ELIZABETH MICHAEL (LULU) AKIWA KWENYE VAZI LA KITENGE

Image
She happen to be my all time fashionista. She is just so perfect when it comes to fashion and Style. Very cute and Intelligent. When Invited to the occasions, she will rock it with the most beautiful look. Haya jamani nimemwaga kiingereza huko juu kwa sababu tu ya kuweka msisitizo. Kiulweli kapendeza sana na mavazi yake yote. Atakayevutiwa na mishono ya kitenge kutoka kwa msanii Lulu basi nae asisite kututumia tuone katokea vipi.

JE KUKU WANAWEZA KUKUONGEZEA KIPATO?

Image
Watu wengi tumekua tunapenda kufuga kuku wawili watatu majumbani kwa ajili ya kitoweo. Wengi wetu tunapenda sana kula nyama ya kuku na hata mayai yake. Ila je tunajua tunaweza kuwafuga kibiashara? Tunajua namna ya kuwapa matunzo bora ili waweze kutuongezea kipato? Siku hizi kuna kuku wa Kienyeji, wakisasa na pia machotara ambayo haya ni mchanganyiko wa kisasa na kienyeji. Sasa ukiwa unataka kufuga kibiashara ni muhimu ujue unataka kufuga kuku kwa ajili ya nyama au mayai. Pia ni muhimu kujifunza changamoto za aina hizi za kuku pamoja na uzalishaji wake na gharama zake ili ujue ni kuku wa aina gani atakufaa kulingana na mtaji ulionao. ukishachagua aina ya kuku kabla ya kuwaleta au kuwazalisha kwa wingi ni vyema kwanza kuandaa makazi yao na uhakikishe ni makazi salama kwao kutokana na wanyama wengine wakali pamoja na maradhi. Pia yawe ni makazi yenye nafasi ili wasibanane pindi watakapo zaliana ili upate fursa ya kupanuka kibiashara. Pia ni muhimu kuwa na vifaa ya kuwalishia na chanjo muh

UFANYAJE ILI KUEPUKA DHANA HASI?

Image
Wengi wetu tumekua tukiisha sana kwa dhana japo imani mbalimbali za dini zimekua zikituonya sana haswa pale tunapokua na dhana hasi. Dhana hasi mara nyingi imekua chanzo cha kuturudisha nyuma na kutufanya tuwe na woga. Dhana hasi zimekua zikigombanisha ndugu na kufarakanisha marafiki. Wengi wetu tumeumizwa na dhana za aina hii na tukajikuta tunamaadui wengi bila sababu za uhakika wala za msingi.  Mara nyingi dhana hii imekua ikisababishwa na wivu , chuki na choyo . Na kwa bahati mbaya sana wengi wetu tunapenda sana kusikia habari mbaya kuhusu flan au kitu flan. Hata action zetu ukiambiwa habari nzuri na mbaya ni tofauti. Na hata waandishi wengi ili kuvutia wasomaji wamejikuta wakiweka kichwa cha habari chenye mawazo hasi ili kuvutia zaidi wasomaji, hii ni kwasababu ubongo wetu unapendelea kujua habari hizi zaidi. Somo la leo linadhamiria zaidi kutufanya tuwe na dhana nzuri, "Thinking Positive" hata ikitokea kuna ubaya basi tengeneza ule ubaya uwe mzuri ili ufanikiwe kwa kuwa

NJIA 5 ZA KUEKEZA PESA ILI KUFIKIA MALENGO YAKO

Image
Mwaka huu unatakiwa uwe ni mwaka wa mafanikio kwetu sote. Ila pia mafanikio hayaji bila malengo. Na malengo nayo hayafikiki bila kuekeza. Kwa kutafakari hilo leo nikaona tuanze mchezo wa kuhamasishana kuekeza. Unachohitaji kufanya ni mambo matano tu ili uweze kuekeza fedha zitakazo kusaidia kufikia malengo yako. 1. Weka Malengo - Hakikisha unajua una malengo gani na kuyafikia malengo hayo unahitaji muda gani. 2. Andaa Bajet - Pia ni vizuri kujua bajaeti yako kwa kwa wiki au mwezi, upate kujua matumizi yako ni kiasi gani na kipato ulichonacho kisha amua utakua anahifadhi pesa kiasi gani 3. Epuka Gharama za ziada - Jitahidi sana kuepuka gharama zisizo za lazima ili uweze kuekeza kama ulivyotamani kuekeza kwa wiki, au kwa mwezi n.k  4. Punguza bili za mwezi - Wote tunajua kuna gharama za lazima ambazo hazikwepeki kama Pango, maji, umeme, maziwa n.k. Gharama hizi ni za lazima ili ukijibana ndani ya budget inaweza kukusaidia kuekeza kwa mujibu wa malengo yako.  5. Fungua Account yenye gh

RAMANI YA NYUMBA YA CHUMBA KIMOJA NA SEBULE

Image
Zamani nilikua nikiendesha blog ya maswala ya ujenzi tu, pamoja na kuachana nayo bado nimekua nikipata maombi kwa wadau mbalimbali wakiomba ramani za nyumba za aina hizi ili wakajenge. Sasa wengi wanapenda nyumba za kisasa ambazo wenyewe tunaita self contain. Hii ya leo ni nyumba ya chumba kimoja cha kulala, sebule iliyoungana na jiko lakini pia ina choo na bafu humo humo. Ukiangalia kwa makini utaona mlango wa chhoni ni wa kioo wa slides, nifanya kioo kwa kuwa mbao mara nyingi ikipata maji huwa inaharibika. Najua sehemu hii muhimu inahitaji privacy so unaweza kuweka pazia zile za bafuni au kioo chako ukaweka kile kizito kisichoonesha. Binafsi napendelea mazia zile za bafuni Ramani hii nimechora mwenyewe tu sina ujuzi sana lakini lengo ni mtu apate ile idea tu. hapa chini nitaweka picha zilizopo kwenye mfumo wa 3D ili picha ionekane vizuri zaidi Picha namba 1 Picha namba 2 Kwa maoni na ushauri, usisite kutuandikia kupitia kwenye comment box.

SABABU 5 ZA KUKUFANYA UFANIKIWE

Image
Vijana wengi sana wamekua na kasumba ya kusema mimi sifanikiwi. Lakini wanashindwa kuelewa mafanikio yanakuja vipi. Wengi wanashindwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwepo malezi, elimu na mazingira. Leo nakupa sababu 5 tu japo zipo nyingi mno ambazo ukitilia mkazo utafanikiwa. 1. Muda/Wakati Mara nyingi tumekua tukiambiwa time is Money. Maana ni kwamba muda unathani kubwa kama pesa. Na mara zote muda ukipita, umepita na hakuna namna utaweza kuurudisha. Hivyo thamani ya wakati ni kubwa kuliko hata pesa yenyewe. Sasa ili kufanikiwa ni lazima ujiweke malengo kwa kuambanisha na muda vizuri. Jitahidi kwenda nawakati katika kila unachofanya. pole pole utaanza kuona maana ya hilo neno "Time is Money" 2. Chukua Hatua Mafanikio hayaji bila wewe kuyatafuta. Ili ufanikiwe ni vyema ukajua unataka nini na unahitaji kufanya nini ili kukiendelea hicho unachokihitaji. Kama ni ajira basi anza kuandika barua na kuzipeleka maofisni, kama ni ujasiriamali jitahidi ujue utafanya nini ili uanze hu